BONGO5.COM – Dubai Kufanya Tamasha Kubwa la Mashabiki wa FIFA

Dubai inategemewa kuhodhi moja kati ya matamasha sita ya mashabiki wa fifa (FIFA FAN FESTIVALS). Tamasha hili la kutazama kombe la dunia linategemewa kuwa na eneo la kutazama mubashara mechi za kombe la dunia katika eneo la heshima la Vista maeneo ya Dubai harbor, eneo lenye uwezo wa kuchukua mashabiki 10,000 kwa siku.

Kila dakika,kila saa ya mpira wa kombe la dunia mwaka huu utaoneshwa mubashara kupitia runinga kubwa zilizotengezwa zenye ukubwa wa mita mraba (square meters) 330, zenye uwezo wa sauti wa 4D.

Kupitia tamasha hili, mashabiki wanategemewa kujihisi kama wapo uwanjani na wataweza kusherehekea kwa pamoja na wengine wote wanaotazama duniani kote. Tamasha hili linalofahamika kwa jina la BUd x FIFA Fan Festival litakua na burudani za Dj katika na mwisho wa mechi, watumbuizaji pamoja na michezo mbali mbali bila ya kusahau vyakula vya kila aina na teknolojia kubwa za kuonesha anga na mengineyo.

Read More @ bongo5.com

Reviews

0 %

User Score

0 ratings
Rate This

Sharing

Leave your comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *